Monday

USIJE MJINI LYRIC

Verse I…
Ogopa matapeli nyumba hii haiuzwi/
Moja ya nembo maarufu hapa mjini mzazi/
Wote tunataka utajiri so zinatungwa mitkas/
Watu wanalia kila siku ka matarumbeta ya arusi/
Jua limeshushwa zaidi mjini/
Na huwaka zaidi mifukoni/
Kila Malaya ana story na zote huwa hazifanani/
kumbuka Zubeda/Yule binti wa Professor/
akashindwa jua atamsaidiaje mjini kuna mengi brother/
wanachapa mpaka ndala/kwenye nyumba za ibada/
sio wote wana pa kulala usidanganywe na luninga/
huku huku kwenye ufisadi waliopo hawataki kurudi/
hata mbunge wa kwenu yupo huko atakuja uchaguzi/
sio wote mambo ni safi wengine wamegomewa na maisha/
wanaona haya watarudije na story walizowahisha/
hakuna shamba hakuna mbuga labda kuwaibia wajinga/
mawazo yatayofanikiwa ni moja ya kumi ya unayoyafuga/
so they say…..

Choras..
yafaa uskize nnayosema/huku kugumu unaweza kupotea/
nananananana (usije mjini)
nananananana (nishakwambia usije mjini)
eeeeeh eeeh (usije mjini)
eeeeeh eeeh (nishasema usije mjini)
eeeeeh eeeh (usije mjini)
eeeeeh eeeh (narudia tena usije mjini)


VERSE II
Maisha ya huku ni mbinde
Yafaa kutumia akili ya kuzaliwa ndio ushinde
Watu wanahustle everyday
Wapunguze makali ya maisha day after day
Kuna wivu,chuki,ghasia,fitina
Watu wako mbio mbio kupoteza muda hakuna
Wanatoroka na wake hata waume wa wenzao
Wengine hawatosheki wanawachapa mpaka watoto zao
Mbwebwe nyingi vyeti feki wengine wakikopa hawalipi
Na si wote wanaosmile ukadhani wako happy
Hawamaanishi ila ubishi
Maisha hayana hata urafiki
Bora bush town uzushi huko undugu huku cash
Town nani hana deni
Kama hauna kazi muda nao hauendi
Na si kila aliye town basi mjanja
Unaweza kuukamata mkwanja
kisha ukaonekana mshamba
usije mjini son

Verse III..
Daisaama samba m’magai/kama mbwai mbwa/
Kuni ni watu jua ndio moto sikutishi mji haufai/
Wamasai hawachungi ng’ombe huku wanalinda magari/
Washaiba deal ya wamakonde mji ulivyokuwa nishai/
Siku hizi hawawindi simba wanasuka dada zetu tu/
Mjini huwezi kuwa mtu kama huna deal ya mkwanja mkuu/
Nafuu huko kuna waganga kweli/huku hata dini ni dili/
Na kuna manyoya cuz mjini sio kuzuri/
Na si kila alie town basi mjanja/
Unaweza ukaukamata mkwanja halafu ukaonekana mshamba/

2 comments:

john elias said...

umetisha kupatamistari kama hii kaka dawson

jokha hamis said...

nakupenda kaka Dawson ntakutafuta