Saturday

Mama wa Mjomba: Dini ya Shetani imempa nafasi kutawala muziki duniani”



Hofu kila kona ni tishio la utawala wa dini ya Shetani. Kwa upande wa muziki, mwana Hip Hop mwenye pesa nyingi zaidi, Shawn Cutter ‘Jay- Z’ au Jigga anatajwa kutawala game kupitia imani hiyo.

Anatajwa zaidi kuamini katika Illuminati au Secret Society (Jamii ya Siri), ingawa lipo tabaka linaloamini kuwa Jigga ni muumini wa Freemasonry. Katika interview tuliyoinasa kupitia YouTube Jigga akizungumzia kuhusishwa kwake na Dini ya Shetani (Illuminati, Freemasonry), anasema kuwa yeye haamini dini, haukubali Ukristo wala Uislamu.

“Watu wanatakiwa kunijua vizuri, waijue imani yangu. Namuamini Mungu, namuamini Mungu mmoja. Siamini dini, Ukristo wala Uislamu.” Mahojiano yapo kama ifuatavyo;

SWALI: Watu wanazungumza wewe ni mfuasi mwaminifu wa Illuminati, Freemason, Dini ya Shetani kitu kama hicho.

JIGGA: No, nashindwa kujua haya yametoka wapi, sijui yameanzaje, kwa kweli siwezi kusema.

SWALI: Watu wanasema kwenye video za nyimbo zako unatumia alama ya Illuminati, labda swali langu ni je, una uhusiano na watu wenye unabii na imani hiyo?

JIGGA: No, siyo mimi. Sijawahi kufanya hivyo. Nimekuwa nikitumia alama hizo kwenye nyimbo zangu kwa sababu naamini zinauza. Labda niseme na watu wajue imani yangu, namuamini Mungu mmoja, siamini dini, siamini jehanamu. Unajua hizi alama huwa nakisia, watu wananiunga mkono. Nafanya shoo na watu tunaonesha alama za kufanana.

SWALI: Umezijuaje wakati ni Jamii ya Siri? Illuminati (secret society).

JIGGA: Yeah, ila kwa sasa ni kundi kubwa. Halafu hizo alama, unajua mimi ni mburudishaji, nazitumia kuburudisha.

SWALI: Ukionesha hizo alama za dini ya shetani mashabiki wanapenda?

JIGGA: Bila shaka.

SWALI: Unafikiri imani hiyo ipo?

JIGGA: Sijui hasa ila watu wanaosafiri duniani wanaweza kufafanua. Sijui kuhusu Dini ya Shetani kwa sababu mimi siyo Tommy Hanks (staa wa filamu ya Illuminati) lakini kuna mtu wangu Young Jeezy ana kitu kuhusu dini hiyo. Nina uhakika Obama (Barack) ana watu hao.

JIGGA NA BEYONCE DINI MOJA
Galacha huyo wa Hip Hop anayeaminika ndiye tajiri zaidi akiwa anamiliki utajiri unaokadiriwa kufikia dola milioni 150 (shilingi bilioni 240), alifunga ndoa na staa wa R&B, aliye memba wa zamani wa kundi marehemu la Destiny’s Child, Beyonce Knowles.

Jigga na Beyonce wamekuwa wakionesha alama za dini ya shetani, hivyo kufanya wote wawili kuwekwa kundi mmoja kwamba like husband like wife wote ni Dini ya Shetani. Wakati mwingine, Beyonce amekuwa akionesha alama za Dini ya Shetani hata katika mazingira ya kawaida, hivyo kuzidi kuuthibitishia umma.

JIGGA NI NGUMU KUWAFANYA WATU WAMUAMINI
Ni ngumu kwa Jigga kuwafanya watu wamuamini yeye siyo Illuminati. Sababu ni hizi;

MOSI: Amesema yeye siyo Mkristo na haamini dini hiyo lakini mbona anavaa msalaba?

PILI: Anasema yeye siyo Freemasonry lakini mbona kwenye wimbo “Run this Town” amejitaja ni muumini wa imani hiyo, pia kwenye video yake amejaza alama za Dini ya Shetani?

TATU: Mbona anapenda kupiga pamba zenye nembo za Illuminati au Freemasonry na mikono yake kuonesha alama hizo?

CHANZO CHA BIFU LAKE NI TUPAC NI ILLUMINATI
Jigga alianza kumshambulia Mfalme wa Hip Hop, marehemu Tupac Shakur ghafla. Hakukuwa na chanzo kinachoeleweka. Katika kukoleza bifu, Jigga akaamua kufanya kazi kwa ukaribu na hasimu wa Tupac wakati huo, marehemu Christopher Wallace ‘Notorious BIG’.

Documentary inayoelezea kifo cha Tupac na dhana ya Illuminati (Tupac’s Death & Illuminati Conspiracy Theory), inafunuliwa kuwa Jigga alianza kumpiga vita gwiji huyo wa mauzo ya Hip Hop baada ya kuponda Dini ya Shetani.

Tupac aliiponda Illuminati. Akasimama mstari wa mbele kuipinga. Hiyo ikawa sababu ya Jigga kumrudi mfalme huyo wa Hip Hop. Documentary hiyo ambayo inahusisha mahojiano na wanamuziki na watu wengine wenye ushawishi nchini Marekani, inasema kuwa kifo cha Tupac kilisababishwa na Illuminati, dini ambayo inatajwa kuwa na nguvu nyingi za giza. Kwamba ili kumuua Pac a.k.a Makaveli The Don, Illuminati walipanda mbegu ya mauaji kwa watu waliotekeleza shambulio la risasi alizopigwa Septemba 7, 1996 kabla ya kufa siku sita baadaye (Septemba 13, 1996).

Inatajwa kwamba ndiyo maana mpaka leo wauaji hawajulikani. Mchongo mzima ulisimamiwa na Jamii ya Siri (Secret Society). Chanzo cha Pac ‘kuidisi’ Illuminati kabla ya Jigga kumgeuka ni kuwa akiwa jela, alipata taarifa kuwa dini hiyo ndiyo ilikuwa inashika mamlaka yote, ilikuwa inaenda kwa kasi na itatawala dunia nzima.

Hilo lilimuudhi Tupac kwa sababu hakutaka kutawaliwa na dini hiyo, kwahiyo akaanza kupambana nayo. Tupac, alikasirika zaidi alipoambiwa kuwa hata kufungwa kwake jela mwaka 1995 ilitokana na nguvu za Illuminati kwa sababu hakutenda kosa ila aliingizwa hatiani.

Skendo ya kubaka iliyompeleka jela ikaelezwa ni kutaka kuchafua sifa yake ya kutetea haki za watu weusi Marekani, kuwapigania wanawake na watoto dhidi ya vitendo vya unyanyasi. Moja ya disi, Tupac anaimba: “Mimi ni muuaji wa Bad Boy, Jay Z atakufa pia.” Kuhusu ujumbe wa Illuminati kummaliza, alijibu: “Sijui hayo maneno kapata wapi, kaambiwa na Papa?”

ANASAIDIA JAMII ‘SANA TU’
Nje ya muziki, Jigga hujihusisha katika shuhuli za uhisani. Agosti 9, 2006 alikutana na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa wakati huo, Kofi Annan ofisini kwake, New York na kumuahidi kufanya ziara ya kutoa elimu ya kuhusu upungufu wa maji duniani.

Alilitekeleza hilo, pia akashirikikiana na Umoja wa Mataifa pamoja na MTV kutengeneza documentary ya kampeni ya maji aliyoipa jina, Diary of Jay-Z: Water for Life, na ilirushwa hewani kwa mara ya kwanza Novemba 2006. Akishirikiana na Sean Combs ‘P Diddy’, Jay-Z alitoa dola milioni 1 (zaidi ya shilingi bilioni 1.4) kulichangia Shirika la Msalaba Mwekundu ili kusaidia waathirika wa Katrina.

ANASHIKA NAMBA TATU KWA MAUZO HIP HIP
Unapowaondoa Tupac na ‘mzungu kichaa’, Eminem, Jay Z ndiye anabaki juu yaw engine wote katika mauzo ya muziki wa Hip Hop. Anakadiriwa kuuza nakala kati ya milioni 40 na 50 duniani kote.

ALBAMU ALIZOTOA
Reasonable Doubt (1996), In My Lifetime, Vol. 1 (1997), Vol. 2… Hard Knock Life (1998), Vol. 3… Life and Times of S. Carter (1999), The Dynasty: Roc La Familia (2000), The Blueprint (2001), The Blueprint2: The Gift & The Curse (2002), The Black Album (2003), Kingdom Come (2006), American Gangster (2007) na The Blueprint 3 (2009).

MADEMU ALIOPANDA NAO KITANDANI
Mtu mzima Jigga kwenye sekta ya mapenzi ni mzuri pia, kwani ameweza kutimiza idadi ya wanawake 11 wanaojulikana aliopanda nao itandani.

Anayetajwa wa kwanza ni Blu Cantrell, Foxy Brown anafuatia, Karrine Steffans anaunga listi, pia Jigga alikosa heshima kwa kutoka na shemeji yake, Lil` Kim ambaye alikuwa tulizo la Notorious BIG enzi za uhai wake. Wengine ni demu gangster, Missy Elliott, rapa mgumu, Trina, Carmen Bryan, Amil All Money, Charlie Baltimore, Shenelle Scott na mke wake, Beyonce Knowles.

HOFU YA KUTAWALA DUNIA
Watu wanazungumza kwamba siku zijazo anaweza kutawala dunia kwa upande wa muziki. Baadhi ya video zinatoka sasa na kumchambua kuwa amepewa mamlaka makubwa na Freemasonry. Mahudhurio ya shoo yake ya hivi karibuni alipochangia jukwaa na Eminem kwenye Uwanja wa Yankees, New York, Marekani yalitia mshtuko baada ya kuingiza watu 52,000. Imetajwa kuwa hao walivutwa na Freemasonry, pia ni zawadi kwake.

HUYU NDIYE ZAY -Z
Jina lake kamilini ni Shawn Corey Carter, alizaliwa Desemba 4, 1969, Bedford Stuyvesant, Brooklyn, New York, Marekani, umri wake kwa sasa ni miaka 40. Alitekelezwa na baba yake akiwa mdogo, hivyo kuishi kwa nguvu ya mama. Akiwa na umri wa miaka 12, alimpiga risasi kaka yake begani kwa kumuibia kidani chake. Alisoma George Westinghhouse Career and Technical Education High School, Downtown Brooklyn ambako alikutana na wakali wengine wa Hip Hop, Big, AZ na Busta Rhymes, baadaye alijiunga Trenton Central High School, Trenton lakini akafeli, hivyo kuanza kukomaa na muziki, pia kujihusisha na kuuza dawa za kulevya.

No comments: