Friday

Diddy apelekwa mahakamni na mfanya kazi wake wa zamani


Sean "Diddy" Combs jana amefunguliwa kesi ya madai ya doal milioni kumi na mbili katika mahakama ya jijini Newyork. Aliyefungua kesi hiyo na mfanyakazi wake wa zamani, ambae anadai kuwa Diddy alimtimua kazini kutokana na umri wake mkubwa na mahitaji yake ya kutibiwa.

Kwa mujibu wa chanzo chetu cha habari kinasema kuwa, mama huyo wa kizungu katika file ya kesi hiyo ameandika kuwa ana umri wa miaka 51 na alizinguana na Diddy kwasababu alimwambia anataka kufanya Hip Surgery. Bi Spero alikua Vice President of Management and Publishing wa BAD BOY RECORDS.

Anasema Diddy alianza kwa kumtoa kwenye cheo chake na ilipofika mwezi wa tatu mwaka huu akampa cheo hicho mwanamke mwingine ambae Bi Spero anadai hana skillz kama zake lakini pia ni mdogo kwake kwa umri wa miaka 10-15.

No comments: